Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sadc: Tanzania imevuka vigezo ukuaji wa uchumi

71845 Uchumi+pic

Sat, 17 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Tanzania imetajwa kuvuka vigezo vya ukuaji uchumi kati ya nchi 16 wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc).

Imetajwa kuwa ni nchi ambayo imefanikiwa kukua kiuchumi kwa muda mfupi.

Hayo yameelezwa leo Jumamosi Agosti 17, 2019 na katibu mtendaji wa Sadc, Dk Stegomena Tax  wakati akifungua mkutano wa kilele wa jumuiya hiyo unaofanyika leo na kesho katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC)

Dk Tax amesema uhimilivu wa uchumi ni nyenzo muhimu katika kuleta maendeleo kwa nchi wanachama na kuzihamasisha nchi nyingine kukua kiuchumi.

"Nchi zilizokidhi vigezo katika nchi wanachama ni nyingi zinafanya vizuri na Tanzania ni nchi pekee iliyofikia kigezo cha asilimia 7 katika ukuaji uchumi. Huu ni mfano wa kuigwa,” amesema Dk Tax.

Chanzo: mwananchi.co.tz