Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sababu mapato Wizara ya Madini kuongezeka hizi hapa

62820 Mapatopic

Sat, 15 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Mapato ya Wizara ya Madini nchini Tanzania  yamepanda kutoka Sh196 bilioni mwaka 2016 hadi Sh310 bilioni mwaka 2018/19.

Takwimu hizo zimetolewa leo Jumamosi Juni 15, 2019 na Waziri wa Madini, Dotto Kiteko katika hafla ya uzinduzi wa soko la kimataifa la madini jijini Arusha.

Amesema maboresho hayo ya mapato yanatokana na mabadiliko ya sheria ya madini na kuanzishwa kwa masoko ya madini.

Akizungumzia mapato ya madini ya Tanzanite, Biteko amesema ambayo yamepatikana Mirerani yameongezeka kutoka kilo 147.7 hadi kufikia kilo 949 huku sababu kuu ikiwa ni kujengwa kwa ukuta kuzunguka mgodi wa madini hayo.

Mkuu wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo amesema Mkoa wa Arusha umejipanga kutekeleza kwa vitendo maagizo ya Rais John Magufuli katika kuboresha sekta ya madini kwa kuanzisha soko la kimataifa.

Pia Soma

Chanzo: mwananchi.co.tz