Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sababu, faida bei ya Dhahabu kuvunja rekodi ya muda wote

Wezi Waiba Dhahabu Ya Sh Bil. 3.8 Sababu, faida bei ya Dhahabu kuvunja rekodi ya muda wote

Thu, 29 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kuadimika kwa Dola za Marekani na kuwapo kwa uchaguzi nchini humo vimetajwa kuwa sababu za ongezeko ya bei ya dhahabu duniani hadi kufikia kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa.

Tovuti ya Trading Economy Jumatano wiki hii ilionyesha kuwa wakia moja ilinunuliwa kwa Dola za Marekani 2,523 (Sh6.85 milioni), kiasi ambacho hakijawahi kufikiwa tangu mwaka 1970 mauzo ya dhahabu yalipoanza kurekodiwa katika tovuti hiyo.

Kuongezeka kwa mauzo haya ni fursa kwa nchi ambazo zinazalisha madini hayo kwani zitakuwa na uwezo wa kupata mapato mengi zaidi yanayotokana na mauzo hayo. Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo.

Mbali na kuongeza mapato ya fedha za kigeni kutokana na mauzo nje ya nchi, pia itaisaidia nchi kupata kodi nyingi kutoka kampuni zinazohusika na mauzo hayo pamoja na mirabaha inayolipwa kwa Serikali.

Akizungumzia ongezeko hilo la bei, Mchambuzi wa uchumi nchini, Oscar Mkude anasema hali hiyo imesababishwa na kushuka kwa mahitaji ya Dola za Marekani duniani kote, uchaguzi katika taifa hilo kubwa huku kukiwa na mfumuko wa bei, kinyume na matarajio ya wengi.

“Ili kutunza thamani ya fedha zake, mataifa yanakwenda kununua dhahabu kulingana na kiwango cha fedha zake, baadaye zikitaka kubadilisha dhahabu kuwa fedha, itakuwa rahisi,” anasema Mkude.

Anasema utaratibu huo hutokea pale watu wanapohisi thamani ya fedha zao inashuka, huwa wanaenda kununua dhahabu, huku akitolea mfano wa kipindi cha Ugonjwa Virusi vya Korona (Uviko 19) dhahabu ilivyopanda bei.

“Sababu ya kufanya hivyo wengi walikuwa wanaamini kufungiwa ndani kulikuwa kunaathiri mwenendo wa uchumi katika maeneo mbalimbali duniani na wengi walianza kununua vitu vya thamani kama dhahabu,” anasema Mkude.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live