Shirika la kuhudumia viwanda vidogo(Sido) Mkoa wa Dodoma limeshauriwa kushirikiana na Shirika la Viwango( TBS), ili kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa na vijana zinakuwa na ubora.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugezi wa Idara ya Ukuzaji Ajira na Ujuzi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ally Msaki kwenye hafla ya kuhitimisha mafunzo ya uanagenzi kwa vijana 147 na kukabidhi vifaa vilivyotolewa na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Maendeleo la Ujerumani GIZ.
Amewataka vijana kutumia ujuzi walioupata kuzalisha bidhaa zenye ubora unaohitajika katika soko la kitaifa na kimataifa