Menu ›
Biashara
Mon, 17 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ripoti mpya ya Shirika la Oxfam inasema utajiri wa Mabilionea 10 wakubwa zaidi umeongezeka maradufu wakati wa CoronaVirus. Mapato ya chini ya Mataifa masikini zaidi duniani yalichangia vifo vya watu 21,000 kila siku.
Shirika hilo limeonya kuhusu kukosekana usawa duniani, likisema hali ya sasa ya kimataifa ya ukosefu wa usawa uliokithiri ni aina ya "ukatili wa kiuchumi" dhidi ya watu na Mataifa masikini zaidi.
Oxfam imetolea mfano mgawanyo wa Chanjo dhidi ya COVID-19, ikisema Mamilioni ya watu bado wangekuwa hai leo kama wangekuwa na Chanjo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live