Menu ›
Biashara
Wed, 26 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
MAMLAKA ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) imeziagiza taasisi za umma kuhakikisha watumishi wote wanaohusika na ununuzi wamepatiwa mafunzo ya namna ya kuutumia mfumo mpya wa ununuzi “National e-Procurement System of Tanzania” (NeST).
Agizo hilo limetolewa na PPRA kupitia taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo hivi karibuni, ambapo taarifa hiyo imesema kuwa, taasisi za umma zinawajibu wa kuhakikisha watumishi wote wanaohusika na ununuzi wamepatiwa mafunzo.
Aidha, taasisi hizo zimetakiwa kuhuisha watumiaji kwa wakati pindi wanapoondoka kwenye taasisi kwa sababu yoyote.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live