Menu ›
Biashara
Thu, 23 Mar 2023
Chanzo: mwanachidigital
Imebainika kuwa Serikali hupoteza mapato kwenye baadhi ya masoko na vituo vya kukusanyia ushuru kutokana na usimamizi na mifumo mibovu iliyopo kwenye maeneo hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) mkoani Mwanza, James Ruge amesema katika ufuatiliaji wa taasisi hiyo uliofanyika katika kipindi cha miezi mitatu kuazia Oktoba hadi Disemba 31, 2022 mkoani humo wamebaini upotevu mkubwa wa mapato ya serikali inayosababishwa na mifumo mibovu.
Chanzo: mwanachidigital