Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nchi saba kushiriki maonesho ya madini Geita

Madini Pic Data Nchi saba kushiriki maonesho ya madini Geita

Thu, 21 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

MKUU wa mkoa wa Geita, Martin Shigella amesema kuwa mataifa saba yamethibitisha kushiriki Maonesho ya Sita ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini mjini Geita. - Shigela amesema hayo leo wakati akizungumuza na waandishi wa habari katika viwanja vya Bombambili mjini Geita yanapofanyika maonesho hayo yaliyoanza Septemba 20 mwaka huu. - Ametaja mataifa yaliyothibitisha kutoa taasisi na kampuni shiriki kwenye maonesho ni Kenya, Malawi, Burundi, China, India, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na wenyeji Tanzania. -

MKUU wa mkoa wa Geita, Martin Shigella amesema kuwa mataifa saba yamethibitisha kushiriki Maonesho ya Sita ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini mjini Geita. - Shigela amesema hayo leo wakati akizungumuza na waandishi wa habari katika viwanja vya Bombambili mjini Geita yanapofanyika maonesho hayo yaliyoanza Septemba 20 mwaka huu. - Ametaja mataifa yaliyothibitisha kutoa taasisi na kampuni shiriki kwenye maonesho ni Kenya, Malawi, Burundi, China, India, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na wenyeji Tanzania. - “Tayari washiriki kutoka Burundi wameshawasili, wanaanza kutembelea maeneo ya wachimbaji wadogo, ni wachimbaji wadogo wameungana na serikali ya Burundi kuja kufanya matembezi hayo. - “Wanakuja kushiriki maonesho haya ili wajifunze mambo mapya ya teknolojia, lakini na wenyewe wajifunze namna ya kuratibu maonesho, na hivo kuwezesha nchi zao pia kuandaa maonesho,” amesema. - Amesema hadi sasa takribani washiriki 400 wamethibitisha kushiriki maonesho ya madini kwa mwaka huu ikiwa ni hatua kubwa ikilinganishwa na mwaka jana ambapo kulikua na washiriki takribani 250. -

Chanzo: www.tanzaniaweb.live