Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Naibu Waziri Mabula ahofia viwanda vya samaki kufa

63342 Pic+mabula

Wed, 19 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Mbunge wa Nyamagana (CCM), Stanslaus Mabula ameitaka Serikali kuangalia sekta ya uvuvi ili kuokoa viwanda vya kusindika samaki visife.

Mabula alikuwa akichangia mapendekezo ya bajeti ya Serikali ya mwaka 2019/2020  bungeni jana Jumanne, Juni 18, 2019.

Amesema wanafahamu dhamira ya Serikali ya kuhakikisha viwanda vyote nchini vinapata nguvu, vijengwe kwa msingi wa uzalishaji na kutoa ajira.

“Mwanza tunaviwanda vya samaki vinane ama tisa, lakini ni viwanda vitatu ama vinne pekee ndivyo vinafanya kazi tena si kwa ufanisi unaotakiwa.

“Lipo tatizo kubwa baada ya operesheni (uvuvi haramu) Serikali ilikuja na bei elekezi ya samaki kuanzia Sh5,500 hadi Sh6,000,” amesema.

Hata hivyo, amesema leo hii kilo moja ya samaki inauzwa kwa bei ya Sh3,800 na kwamba, ili kumvua samaki anagharimu lita moja ya mafuta ambayo ni Sh2,800.

Pia Soma

“Serikali imeiacha sekta hii ya samaki kwa kuwaachia wenyewe wafanyabiashara na wenye viwanda wahangaike kutafuta masoko, wahangaike kutafuta bei wahangaike kuona namna wanavyoweza kuendesha viwanda husika,” amesema Mabula.

Amesema kiwanda kimoja kilichokuwa na uwezo wa kuajiri wafanyakazi 700 hivi sasa kinaajiri 50 hadi 90 kwa shifti moja na kilichokuwa na uwezo wa kupata tani 70, leo kinapata tani 10.

Mabula amesema wafanyabiashara wadogo wanapenda kuwepo kwenye sekta hiyo bali ni kwa sababu hakuna kazi za kufanya na ndiyo maana wanatafuta mitaji ya Sh200,000 ili waweze kuuza biashara yoyote na hivyo kujikimu na maisha.

Chanzo: mwananchi.co.tz