Dar es Salaam. Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua mkopo wa bima unaoanzia Sh1 milioni ukiwalenga zaidi wafanyabiashara walio katika sekta ya uchukuzi.
Akizungumza na washiriki wa mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (Tatoa) jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Biashara wa NBC, Elvis Ndunguru amesema mkopo huo utaanzia Sh1 milioni hadi Sh300 milioni.
Amesema mkopo wa bima wa NBC ni maalumu kwa ajili ya bima za biashara zote zikiwemo magari, bidhaa zilizo safarini, majanga ya moto, ujambazi, hatari za barabarani na ajali kwa wafanyakazi.
“Mtu yoyote mwenye mahitaji ya bima akiwa na rasilimali zozote kama vile nyumba ana sifa ya kupata mkopo huu bila kuwa na dhamana yoyote.”
“Utalipia miezi miwili ya bima yako NBC na benki tutalipia miezi 10 inayobaki kwa wakala kwa niaba yako, wewe utailipa benki kila mwezi kidogo kidogo. Mkopo huu una riba ndogo kuliko mikopo yote inayotolewa na benki,” amesema Ndunguru.
Mkurugenzi huyo amesema uamuzi wa kuanzisha huduma hiyo inayowalenga wafanyabiashara umetokana na kasi ya utendaji wa serikali ikiwemo kuondoa kero zilizokuwa zikiizorotesha sekta ya uchukuzi nchini.
Pia Soma
- Magufuli asema alitamani kufukuza viongozi wote wa Morogoro
- Samia amtahadharisha RC mpya Morogoro
- Mbunge Mtulia aanza amshaamsha kuelekea uchaguzi serikali za mitaa
Kamwewle alitolea mfano hivi karibuni benki hiyo ilisaini makubaliano na Shirika la Posta Tanzania kwa ajili ya kuweka ofisi kwenye kila tawi la shirika hilo lililopo nchini