Balozi wa zao la pamba nchini, Aggrey Mwanri amewataka viongozi wa kata na vijiji kuwachukulia hatua wakulima wa pamba watakaobainika kuchanganya mazao mengine na zao hilo, kwani inasababisha kutokuwa na mavuno ya kutosha.
Balozi wa zao la pamba nchini, Aggrey Mwanri amewataka viongozi wa kata na vijiji kuwachukulia hatua wakulima wa pamba watakaobainika kuchanganya mazao mengine na zao hilo, kwani inasababisha kutokuwa na mavuno ya kutosha. Mwanri ametoa maagizo hayo akiwa kwenye Vijiji vya Lubili, Ilalambogo na Isenegeja akiwa katika mwendelezo wa ziara yake Wilaya ya Misungwi, mkoani Mwanza akitoa elimu na kanuni za kuzingatia kwenye kilimo hicho ili kiwe na tija.