Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtafiti wa kilimo ayataja maeneo matatu yanayoweza kufanikikisha sekta ya kilimo Tanzania

59361 Tafitipic

Fri, 24 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mtafiti wa Masuala ya Kilimo wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Dk Anna Temu amesema kuna haja ya kuangalia kwa undani suala la  masoko ili kilimo kiweze kufanya vizuri nchini.

Dk Temu ametoa kauli hiyo, leo Alhamisi Mei 23,2019 wakati akizungumzia suala la msaada na huduma kuhusu sekta ya kilimo katika mjadala wa Jukwaa la Fikra uliokuwa na mada ya ‘Kilimo, Maisha yetu’ ulioandaliwa kampuni ya Mwananchi Communication ltd (MCL) ikishirikiana na ITV na radio One.

Jukwaa hilo la nne linahudhuriwa na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga na wadau wa mbalimbali wa maendeleo na kilimo , likiwamo Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (FAO).

Dk Temu ametaja masoko hayo kuwa ni la ardhi, rasilimaliwatu,  teknolojia na huduma za ugani akisema yakitiliwa mkazo kilimo kitafanikiwa.

“ Kuna haja ya kuangalia soko la rasilimaliwatu, lazima tujue  vijana tulio nao  uwezo wao kwenda kwenye kilimo. Soko la wajasiriamali watu tulilonao haliwezi kuwafikia  wakulima kwa ufanisi,”  amesema  Dk Temu.

Chanzo: mwananchi.co.tz