Menu ›
Biashara
Wed, 16 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mradi wa ujenzi wa reli ya Kisasa (SGR) inayoanzia Mwanza hadi Isaka mkoani Shinyanga yenye urefu w Kilometa 341 umefikia asilimia 17 huku ukitarajiwa kukamilika Machi 2026.
Mradi huo uliyoanza Mei 2021 unatekelezwa na Kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) kwa gharama ya zaidi ya Sh3.12 trilioni.
Akizungumza jana Novemba 15,2022 alipokagua mradi huo, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Atupele Mwakibete amewahakikishia wananchi kuwa mradi huo utakapokamilika ndani ya muda wa mkataba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live