Mfanyabiashara na bilionea maarufu nchini, Mohamed Dewji 'Mo' amempa kongole mmiliki wa mtandao maarufu DUniani wa Twitter, Elon Musk kwa uamuzi wake wa kubadilisha logo ya kampuni hiyo kutoka logo ya ndege mpaka logo ya 'X'.
Mo Dewji ambaye pia ni mwekezaji wa Simba amesema amependa ubunifu wa Elon kwenye kubadilisha logo hiyo.
"Naipenda herufi X, inaonyesha kitu kisichojulikana, katika hesabu siku zote tulitaka kujua X, nampenda pia Malcolm X. Ndiyo maana nikakiita kinywaji changu Mo Xtra. Umefanya vizuri Elon Musk Tunatazamia kujihusisha zaidi na mtandao X," amesema Mo Dewji.
Una maoni gani?