Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkenda ataka mkakati viwanda vya mbolea

32b279bf1ac132fad13ea564f28cb1df.jpeg Mkenda ataka mkakati viwanda vya mbolea

Tue, 8 Jun 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

WIZARA ya Kilimo imeitaka bodi na menejimenti ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) iandae mkakati wa kupata mbolea nchini kwa bei nafuu.

Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda ametoa agizo hilo jana alipozungumza kwenye kikao kazi alipoitembelea taasisi hiyo kuona utendaji na upatikanaji wa mbolea. Alikuwa katika ziara ya kikazi ya siku moja Dar es Salaam.

Aliitaka TFRA pia iandae mkakati wa uanzishwaji viwanda vipya vya mbolea nchini.

Alisema bodi na menejimenti ya TFRA ina jukumu la kuhakikisha uzalishaji mbolea nchini unapewa kipaumbele ikiwamo kuongeza viwanda ili pembejeo hiyo ipatikane kwa urahisi na kwa bei nafuu ili kila mkulima amudu kuinunua.

Alisema bodi na menejimenti ya TFRA wanapaswa kubuni mkakati wa namna bora ya kuongeza uwekezaji nchini ili wakulima wawe na uhakika wa kupata mbolea kwa bei nafuu.

Profesa Mkenda aliwataka watumishi wa TFRA waongeze udhibiti kwenye usimamizi wa ubora wa mbolea hasa kwenye mikoa yenye matumizi makubwa ya mbolea.

Chanzo: www.habarileo.co.tz