Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkataba wa Barrick na Serikai watajwa kuwa na tija zaidi

AVvXsEgjLQA1aSO7oDWuHJb28YySwcG Qhm5fz8e L EJHt UPPJo N1PEhHEMIyPLBtZpD18l5VpRuk NN9vnMafpItH19NmYpt Mkataba wa Barrick na Serikai watajwa kuwa na tija zaidi

Wed, 26 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa ubia baina ya Serikali na kampuni ya Barrick (Barrick Gold Corporation) uliounda kampuni tanzu ya Twiga (Twiga Minerals Corporation Limited) umeleta tija kubwa katika sekta ya madini nchini.

Waziri Dkt. Biteko ameyasema hayo Januari 25, 2022 alipotembelea mgodi wa Bulyanhulu uliopo Halmashauri ya Msalala Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ikiwa ni miongoni mwa migodi inayoendeshwa na kampuni ya Twiga kwa ubia baina ya Serikali yenye asilimia 16 na Barrick yenye asilimia 84.

Amesema ubia huo umechochea fursa zaidi za ajira kwa watanzania ambapo katika mgodi wa Bulyanhulu zaidi ya asilimia 96 ya wafanyakazi ni watanzania ambapo asilimia 41 wanatoka katika maeneo yanayozunguka mgodi.

Aidha Waziri Dkt. Biteko ameongeza kuwa hatua hiyo imechochea ongezeko la makusanyo ya Serikali katika Sekta ya madini kutoka chini ya shilingi 115 mwaka 2015 hadi kufikia shilingi bilioni 528 mwaka 2020/21 huku pia ikifungua ubia zaidi baina ya Serikali na makampuni mengine.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live