Meya wa Jiji la Mwanza Sima Constantine pamoja na Mkurugenzi wa Jiji Yahaya Sekiete wamekabisdhi hundi ya Tsh. milioni 449.7 kwa vikundi 45 Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemevu ikiwa ni 10% ya fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji.
Wakati wa kukabidhi Meya Sima ameeleza namna wanafuika wa mkopo wanatakiwa kuziheshimu fedha hizo kwa uaminifu na kuhakikisha wanarejesha kwa wakati ili kutoa nafasi kwa makundi mengine kunufaika na mkopo unaotolewa.
Wanufaika wa fedha za mkopo wa 10% za Halmashauri watatakiwa kurejesha fedha hizo ndani ya mwaka mmoja hadi mitatu kulingana na kiwango cha fedha kilichotolewa kwa kikundi husika.