Ofisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT Center Limited, Godfrey Kirenga: Zao la mahindi katika mkoa wa Iringa, Mbeya na Songwe unaweza kufikia ufanisi w zaidi ya tani 10 kwa hekta.
Tumefanya mbinu hizi kwa kutumia wakulima kama 2000 na wameweza kufikia wastani wa tani 7 hadi 8 kwa hekta, hili ni ongezeko kubwa na ni ishara kuwa inawezekana.
Mfano mwingine ni Mkulima wa viazi mviringo mkulima wastani wake ni kati ya tani 5 hadi 7 kwa hekta lakini akitumia mbinu za kilimo bora tumeweza kuwafikisha hadi wastani wa tani 28 katika mkoa wa Njombe.
Katika hao wakulima kuna wengine wamefika hadi tani 50 kwa hekta kwa viazi mviringo na wako juu ya viwango vya dunia ambavyo ni tani 40 kwa hekta.”