Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Meli za mizigo zagongana

Screenshot 2021 12 14 At 11.06.10 660x400.png Meli za mizigo zagongana

Tue, 14 Dec 2021 Chanzo: millardayo.com

Meli mbili za mizigo ziligongana Kusini mwa Sweden, na kusababisha kupinduka kwa meli moja na mabaharia wawili kuzama baharini, kulingana na mamlaka ya baharini ya Sweden.

Ajali hiyo ilitokea majira ya saa 2:30 saa za kimataifa, katika Bahari ya Baltic kati ya ncha ya kusini ya Sweden na kisiwa cha Denmark cha Bornholm kati ya meli ya mizigo ya Uingereza na meli ya Denmark, ambayo ndiyo iliyopinduka, msemaji wa mamlaka hiyo, Carl- Johan Linde ameliambia shirika la habari la AFP

Watu kadhaa wanahofiwa kuwa majini na operesheni kubwa ya uokoaji inaendelea, Operesheni kubwa ya uokoaji inayohusisha boti tisa na helikopta inaendelea, katika maji baridi sana, yenye digrii nne tu.

Chanzo: millardayo.com