Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi na Bahari Kuu kwa kushirikiana na Mmiliki wa Meli mbili za kitanzania aina ya mishipi wamesaini mkataba wa Ushirikiano katika kuimarisha ulinzi kwenye meli za uvuvi hasa wavuvi wanapokwenda kufanya shughuli zao uvuvi kwenye Bahari kuu.
Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi na Bahari Kuu kwa kushirikiana na Mmiliki wa Meli mbili za kitanzania aina ya mishipi wamesaini mkataba wa Ushirikiano katika kuimarisha ulinzi kwenye meli za uvuvi hasa wavuvi wanapokwenda kufanya shughuli zao uvuvi kwenye Bahari kuu. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam mara Baada ya Utiaji saini wa mkataba huo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi na Bahari Kuu Dk. Emmanuel Sweke amesema Mkataba waliyousaini unakwenda kuimarisha ulinzi kwenye meli za uvuvi ikiwemo ufungaji wa camera kwenye meli ili kuona kila kitu kinachoendelea hasa wavuvi wanapokuwa baharini wakivua samaki.