Bashe amesema hayo leo bungeni alipokuwa anajibu swali la mbunge wa Nkasi Kaskazini, Aida Khenani, lililohoji kwanini serikali isibadili utaratibu wa mikopo ya pembejeo kwakuwa ule unaotumika sasa unawaumiza wakulima kwa kuwatoza riba kubwa.
“Hatua hii itasaidia kutambua changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi ikiwemo kupunguza riba pamoja na kuweka utaratibu wa kumsaidia mkulima katika kurejesha mkopo kulingana na mapato ya mkulima kwa msimu wa kilimo” amesema Bashe.
Bashe amesema kuwa wamepanga kuhamasisha sekta binafsi kuanzisha vituo vya kukodisha zana za kilimo ili kusogeza karibu upatikanaji wake kwa wakulima