Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema, Serikali imeagiza ndege nyingine aina ya Dash 8 ili kuliongezea uwezo zaidi Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) liweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi
Akitoa taarifa kuhusiana na ujio wa ndege mpya ya ATCL aina ya Boeing B787-8 Dreamliner iliyotua leo nchini, Profesa Mbarawa amesema ujio wa ndege hiyo hapo mwakani utawezasha shirika hilo kuwa na ndege 16 mpya na kwamba ndege yake moja ya zamani imeharibika
Amesema, lengo la Serikali ni kuhakikisha ndege hizo zinakuwa na mchango kwenye uchumi wa taifa kwa kuanzisha safari zenye tija na maslahi kwa umma na kuiletea nchi maendeleo.