Dodoma. Serikali ya Tanzania imesema mauzo ya korosho nje ya nchi yalikuwa Dola 196.5 milioni za Marekani mwaka 2018 ikilinganishwa na Dola 529.6 milioni mwaka 2017, sawa na upungufu wa asilimia 62.9.
Hayo yameelezwa leo Alhamisi, Juni 13, 2019 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipowasilisha taarifa ya hali ya uchumi wa Taifa kwa mwaka 2018 na mpango wa maendeleo wa Taifa wa mwaka 2019/20.
Dk Mpango amesema upungufu huo umetokana na kupungua kwa kiasi cha korosho kilichouzwa nje kutoka tani 329,400 mwaka 2017 hadi tani 120,200 mwaka 2018 sawa na asilimia 63.5.
“Aidha, bei ya korosho katika soko la dunia ilipanda kwa asilimia 1.6 kutoka Dola 1,607.7 za Marekani kwa tani moja mwaka 2017 hadi Dola 1,634.2 mwaka 2018.