Ushahidi wa ki-axiology umebainisha kwamba binadamu wamekuwa wakifurahia vyakula vya unga wa ngano au vya kukaanga tangu enzi na enzi.
Tangu watu wa kale walipovumbua kikaangio hadi sasa ambapo CNN kupitia CNN Travel wameyataja maandazi kutoka Afrika Mashariki kama miongoni mwa vyakula 30 bora zaidi vya kukaanga duniani.
Sehemu ya maelezo yao kuhusu maandazi kwenye orodha hiyo yanasomeka kama ifuatavyo; "Sawa na vyakula vingi vitamu vilivyokaangwa maandazi huitwa majina mengi kwenye pwani ya Afrika Mashariki."
Baadhi ya vyakula vingine vilivyotajwa kwenye Top 30 ni pamoja na tempura ya Japan, hushpuppies ya Amerika Kusini, churros ya Hispania, Ureni na Latin America, Jalebi ya India, Zucchini ya Italia na cronuts za Marekani. #TanzaniaWeb.Com