Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mali makontena ya Makonda zaanza kupigwa mnada

14975 Makontena+pic TanzaniaWeb

Sat, 1 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mnada wa mali zilizomo ndani ya makontena 20 ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, unaendelea na tayari wateja wameshakagua bidhaa na wanashindana kununua.

Bidhaa zilizomo kwenye makontena hayo ni samani za ofisini kama vile viti, meza na makabati.

Mkurugenzi wa kampuni ya Yono Auction Mart, Scholastica Kevela amewataka wanunuzi kuwa na vitambulisho, leseni ya gari na pasi ya kusafiria.

Hata hivyo, bado wateja wengi hawajafikia bei zinazotakiwa.

Bei zinazotajwa ni kati ya Sh6 milioni hadi 15 milioni.

Awali Mkurugenzi Mwenza wa kampuni hiyo, Yono Kevela aliwaambia waandishi wa habari kuwa kuna matumaini ya bidhaa zote kununuliwa tofauti na mnada wa awali uliokosa wateja.

Mnada huo unafanyika katika bandari kavu ya Malawi Cargo.

Chanzo: mwananchi.co.tz