Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Makontena ya Makonda kaa la moto, yakosa mnunuzi kwa mara ya tatu

16292 Makontena+pic TanzaniaWeb

Sun, 9 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam.  Kwa mara ya tatu mfululizo mnada wa makontena 20 yaliyoagizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda umefanyika bila mafanikio, baada ya wateja kushindwa kufika bei.

Mnada huo umefanyika leo Jumamosi Septemba 8, 2018 katika  bandari ya kavu ya DICB, jijini Dar es Salaam.

Wakizungumza  baada ya mnada kumalizika bila makontena hayo kununuliwa, wateja  waliojitokeza wamesema bei iliyowekwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ni kubwa kwa kuwa wanajua thamani ya samani zilizomo katika makontena hayo.

Jimmy Cosmas amesema kontena moja halizidi Sh30 milioni lakini TRA wanauza kontena moja kwa Sh60milioni.

"Wanunuzi wapo wakishusha bei yatanunulika. Mimi ninafanya biashara najua kwa bei hiyo waliyopewa wasitegemee kuuza" amesema Jimmy.

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya udalali ya Yono,  Scolastica Kivela amesema wanatekeleza jukumu walilokabidhiwa na kwamba  wanasubiri maelekezo mengine ya TRA kujua nini cha kufanya.

“Kama mnavyoona samani hazijanunulika wateja wamejitokeza ila bei wanayoishia ni Sh20milioni hadi Sh30milioni, tunasubiri maelezo mengine ya TRA,” amesema.

Soma Zaidi:

·Makontena 10 ya Makonda yazua utata mpya mnadani

Mali makontena ya Makonda zaanza kupigwa mnada



 

 

Chanzo: mwananchi.co.tz