Arusha. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuzungumza na wanahisa zaidi ya 1,000 wa benki ya CRDB jijini Arusha.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Mei 15, 2019 mkurugenzi mkuu wa CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema Waziri Mkuu atazungumza na wanahisa wa benki hiyo ijumaa.
"Kwa mara ya kwanza, Waziri Mkuu atafungua semina ya wanahisa wa benki kutoka maeneo mbalimbali nchini siku ya Ijumaa ambapo licha ya kujadili fursa za kiuchumi watajadili mipango ya benki," amesema.
Amesema baada ya ufunguzi huo,wanahisa wa benki hiyo watakuwa na mkutano mkuu ambao utajadili pendekezo la gawio la wanahisa mwaka 2018.
Nsekela amesema wanahisa pia watapokea taarifa za fedha,watachaguwa wajumbe watano wa bodi na kuidhinisha wakaguzi wa hesabu.
"Tunaomba wanahisa kujitokeza kwenye mkutano huu muhimu kujadili maendeleo ya benki " amesema
Pia Soma
- Waziri atoa matumaini ya kuuza korosho
- Kipindi cha televisheni cha udaku chafutwa baada ya mgeni kufariki saa chache baada ya kuhojiwa
- VIDEO: Huenda hizi zikawa sababu ya Makalla kuondolewa ukuu wa mkoa
Mkurugenzi wa masoko wa CRDB, Tully Mwambapa amesema semina na mkutano mkuu wa benki hiyo ni fursa nzuri ya wanahisa na wateja wa benki hiyo kujua mikakati ya benki na maendeleo yake.