Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, John Magufuli amewaeleza wamiliki wa viwanda vya mabomba nchini kuwa Serikali inapotaka kuwalinda lazima na wao waangalie namna biashara inavyokwenda.
Mkuu huyo wa nchi ameeleza suala hilo, akiwa na maana kuwa wamiliki hao waangalie na suala la bei la bidhaa hiyo kama wanataka iwalinde.
Rais Magufulia ametoa kauli leo Jumatatu Septemba 10, 2019 wakati akizundua Kiwanda cha kutengeneza mabomba cha Pipe Indrustries Limited kilichopo Vingunguti.
“Wenye viwanda angalieni suala la bei zenu. Inawezekana bei za mabomba yenu ni ghali kuliko yanayotoka nje ya nchi. Naambiwa wakati mwingine bei za mabomba nchini zipo juu kuliko yanayoagizwa kutoka nje. Bomba linatoka nje linalipiwa kodi lakini bado linakuwa na gharama nafuu kuliko lililotengenezwa hapa Vingunguti,”amesema Rais Magufuli.
Amewaambia kuwa Serikali inapotaka kuwalinda lazima waangalia suala hilo, kwa kuwa biashara ni ushindani huku akiwataka kufanya uchambuzi kuhusu ubora na bei za mabomba hayo.
Amesema jambo jema tayari Serikali imeshaweka utaratibu mzuri kwenye malighafi zinazoagiwa kwa ajili ya kuwarahisishia katika uzalishaji.
Habari zinazohusiana na hii
- Rais Magufuli amtaja Tundu Lissu, asema alitelekeza jimbo lake
- Magufuli akunwa na Balozi wa Ufaransa, aagiza apewe vitabu vya Kiswahili
- LIVE: Magufuli atua JNIA kuzindua Rada zitakazookoa fedha, usalama Dar
- Rais Magufuli amsifia Waziri Bashungwa