Menu ›
Biashara
Fri, 16 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaanza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha asilimia tano kwenye magari yenye uwezo wa injini (Engine Capacity) wa kati ya 1,000 CC hadi 2,000CC.
“Ushuru huo utatozwa ili kuwianisha na magari mengine yenye ukubwa unaofanana. Magari hayo ni yale yanayotambuliwa kwenye H.S Codes 8703.40.00, 8703.50.00, 8703.60.00 na 8703.70.00,”amesema
Dk Nchemba ameyasema hayo leo Alhamis Juni 15, 2023 akiwasilisha hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2023/2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live