Rais John Magufuli kesho kutwa atashuhudia utiaji saini wa kuanza kwa mradi wa uchimbaji wa madini ya Nikel wilayani Ngara, madini hayo yanapatikana katika eneo la Kabanga.
Rais John Magufuli kesho kutwa atashuhudia utiaji saini wa kuanza kwa mradi wa uchimbaji wa madini ya Nikel wilayani Ngara, madini hayo yanapatikana katika eneo la Kabanga. Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbasi amesema serikali kwa sasa ipo kazini na inaendelea na kazi kubwa ya utatuzi wa kero za wananchi huku akibainisha miradi yote mikubwa nchini kama vile Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere na Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) inaendelea vema.