Maonyesho ya Kilimo Nanenane 2023 yamefunguliwa leo Agosti Mosi katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango.
Maonyesho ya Kilimo Nanenane 2023 yamefunguliwa leo Agosti Mosi katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango. Mkuu wa Wilaya ya Ludewa, Victoria Mwanziva, amewakaribisha wananchi na wakulima kwenye maonyesho hayo kutembelea banda la Halmashauri ya wilaya hiyo, kukutana na wataalam wa kilimo, maofisa ugani, wadau wa kilimo na wajasiriamali kutoka Ludewa ili kupata kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo elimu ya kilimo, shamba darasa la mazao mbalimbali, kizimba cha samaki, ufugaji wa kuku, ufugaji wa nyuki.