Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Lipumba ahoji JWTZ kujihusisha na korosho, Serikali yamjibu

63903 Cufpic

Mon, 24 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahimu Lipumba amesema Serikali ya Tanzania ilifanya kosa kuingiza jeshi kwenye biashara ya korosho kwani shughuli hiyo ilipaswa kufanywa na sekta binafsi.

Amesema jeshi lina kazi ya kulinda mipaka ya nchi na sio kuhusishwa kwenye masuala ya biashara kwani Serikali inatakiwa kujenga mazingira ya sekta binafsi kuwekeza kwenye shughuli za kibiashara.

Profesa Lipumba ameyasema hayo leo Jumamosi Juni 22,2019  jijini Dar es Salaam wakati wa kongamano la haki na furaha kwa wote lililowakutanisha viongozi na wanachama wa chama hicho.

“Kuna mambo ambayo sekta binafsi inaweza kuyafanya, huna haja ya kupeleka jeshi kwenye biashara ya korosho, mtu anayekutakia mema na kukuheshimu ni anayekueleza ukweli. Hatuna sababu kwa Serikali ambayo haiwekezi vizuri kwenye afya na elimu kuingia kwenye biashara huko inatakiwa kuweka mazingira mazuri,” amesema

“Kazi ya kweli ni kulinda mipaka ya nchi, sio kwenda kununua korosho, tumefanya makosa na sasa tujirekebishe kwa kuhakikisha wakulima waliouza korosho wanalipwa fedha zao, sio kuwarudishia korosho kwamba zimeharibika

Hata hivyo, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Mathew Mtigumwe akizungumza na Mwananchi kuhusu hoja hiyo ya Profesa Lipumba alisema jeshi halikuingia kwenye korosho kwa ajili ya kufanya biashara bali kuzikusanya katika sehemu ya usalama huku ikiacha biashara ikifanywa na watu binafsi.

Pia Soma

Katika mkutano huo wa CF, Makamu Mwenyekiti wake-Bara, Maftaha Nachuma amesema chama hicho ndiyo kilianzisha ajenda ya kutetea rasilimali za nchi

“Sisi ndiyo waanzilishi wa kwanza wa kutetea rasilimali katika nchi hii, sisi sio kazi yetu kupinga kila kitu ndani ya Bunge, mambo ya msingi yote tunaunga mkono kwa sababu yanaleta maslahi  mapana kwa watanzania na wananufaika,” amesema

Nachuma ambaye pia ni Mbunge wa Mtwara Mjini amesema, “Kuanzia leo tunazaliwa upya na hatutaki tena kuonewa, wale wote ambao hawaitakii mema CUF ila wako kwa maslahi binafsi watambue kuwa nchi hii ni ya vyama vingi.”

Chanzo: mwananchi.co.tz