Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kinaunganishwa na Mamlaka ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) ili kuunda taasisi moja itakayoratibu uwekezaji wa sekta binafsi wa ndani na kutoka nje ya nchi.
Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kinaunganishwa na Mamlaka ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) ili kuunda taasisi moja itakayoratibu uwekezaji wa sekta binafsi wa ndani na kutoka nje ya nchi. Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amesema leo Jijini Dar es Salaam na kusisitiza mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan la kutaka kufanyika mageuzi makubwa katika uendeshaji wa mashirika na taasisi za umma.