Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kampuni kutoa hadi Tsh. Milioni nne biashara ya mende

Mende Biz Biz.jpeg Kampuni kutoa hadi Tsh. Milioni nne biashara ya mende

Sun, 19 Jun 2022 Chanzo: BBC

Kampuni ya kudhibiti wadudu iliyoko North Carolina inalipa $2,000 ili kuwaruhusu wamiliki wa nyumba kuwaachilia mende majumbani mwao.

Kampuni hiyo, inayoitwa The Pest Informer, ilisema kwenye tovuti yake kwamba inatafuta familia tano hadi saba ambazo zingeruhusu mafundi wake wa wadudu kuachilia hadi mende 100 ndani ya nyumba zao ndani ya siku 30.

Vigezo vilivyowekwa na kampuni kwa wale wanaotaka kushiriki katika utafiti huu ni pamoja na: Mwenye nyumba anahitajika kupata kibali cha maandishi, ambacho lazima awe na umri wa angalau miaka 21, na mali lazima iwe katika jiji la Marekani.

Kampuni hiyo ilisema mbinu hii itairuhusu kujifunza "mbinu mahususi za kudhibiti wadudu."

Utafiti utachukua hadi siku 30 na utahitaji mafundi kupiga picha kinachoendelea.

Chanzo: BBC