Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Huu ni muongo wa kujilisha na kuwalisha wengine kibiashara - Majaliwa

Huu Ni Muongo Wa Kujilisha Na Kuwalisha Wengine Kibiashara   Majaliwa.png Huu ni muongo wa kujilisha na kuwalisha wengine kibiashara - Majaliwa

Thu, 18 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (Mb), ameipongeza sekretarieti ya mradi wa Sera na Maboresho ya Sekta ya Kilimo (ASPIRES) na washirika wake kwa kuandaa Mkutano wa 10 wa Sera ya Kilimo – AAPC.

“Muongo wa Marekebisho ya Sera yenye Athari: Kuendesha Mifumo Inayostahimilivu, Jumuishi na Endelevu ya Chakula” ni kaulimbiu iliyotawala mkutano wa tarehe 17 Aprili 2024, kwenye Ukumbi wa Mabeyo mjini Dodoma.

“Ninahimiza majopo yenu kufikiria zaidi ya uzalishaji wa chakula, haswa kutafakari juu ya mfumo wa lishe kwa ujumla. Elimu zaidi inahitajika ili kukabiliana na utapiamlo, upungufu wa damu na magonjwa mengine yasiyoambukiza yanayohusiana na lishe,” alisema Mhe. Majaliwa.

Wakati huo huo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) alisema kuwa Mkulima anahitaji kuhakikishiwa mifumo ya umwagiliaji, masoko na mbegu bora ili kuzuia upotevu wa mazao au uzalishaji.

“Tumekuwa tukiwahimiza washirika wetu wa maendeleo kuhakikisha kwamba msaada wao unaleta athari katika kushughulikia mahitaji ya mkulima kwenye mnyororo wa thamani kama vile mifumo ya umwagiliaji, vifaa vya usimamizi baada ya mavuno au upatikanaji wa masoko,” Mhe. Bashe.

Mkutano huo unawakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wakulima na taasisi za fedha. Washiriki watajikita katika kupitia upya mageuzi ya sera ya kilimo katika miaka 10 iliyopita; kushiriki katika mijadala mahiri na ushauri wa jinsi ya kuboresha zaidi sekta ya kilimo.

Kuhusu mjadala kuhusu mada kuu ya mkutano huo, Mkurugenzi wa AGRA nchini Tanzania, Bw. Vianey Rweyendela alisema kuwa ni muhimu kwa Tanzania kutumia vyema uwezo wake na kujiweka kama nchi ya kapu la chakula. Hii itaongeza uwezo wake wa kuwa na mabilionea wa kikanda kupitia sekta ya kilimo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live