Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba amesema katika mwaka wa fedha 2023/24, Serikali itaendelea na utekelezaji wa miradi ya kielelezo. Miradi hiyo inajumuisha:
Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba amesema katika mwaka wa fedha 2023/24, Serikali itaendelea na utekelezaji wa miradi ya kielelezo. Miradi hiyo inajumuisha: 1. Ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa (Standard Gauge Railway - SGR); 2. Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere – MW 2,115; 3. Kuboresha Shirika la Ndege Tanzania (ATCL); 4. Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia kuwa Kimiminika (LNG) – Lindi; 5. Kufua Umeme wa Maji wa Ruhudji (MW 358) na Rumakali (MW 222) – Njombe; 6. Daraja la JPM - Kigongo – Busisi (Mwanza); 7. Ujenzi wa barabara na Madaraja Makubwa; 8. Kuendeleza Kanda Maalumu za Kiuchumi ikiwemo Eneo Maalumu la Uwekezaji Bagamoyo; na 9. Programu ya Kuendeleza Ujuzi Adimu.