Tume ya Ushindani (FCC) imewaomba wafanyabiashara wadogo na wakubwa kuepuka na kuachana na tabia ya kuuza au kusambaza bidhaa bandia kwani adhabu zitachukuliwa kwa kampuni au mtu binafsi atakayefanya hivo.
Akitolea ufafanuzi juu ya suala la bidhaa bandia katika Viwanja vya maonyesho ya sita ya tenchnojia ya Madini yanaendelea kufanyika Mjini Geita Afisa Mkaguzi, Ofisa mfuatiliaji wa bidhaa bandia sokoni Mgasi Ilalindimiya amesema kupitia sheria ya alama za bidhaa imeelezekeza kutoa adhabu pale watapokuta mfanyabiashara anauza bidhaa bandia hivyo wafanyabiashara waepuke bidhaa hizo
"Kutoa Elimu kwa umma ni wajibu wetu kwa mujibu wa sheria ndiyo maana wanazunguka kila Eneo la kuhakikisha watu wanazindambua bidhaa BANDIA"
"Ni wajibu pia wetu kuhakikisha hakuna bidhaa bandia yeyote inayozalishwa wala kusambazwa au kuuzwa.”
Amesema FCC ni chombo muhimu katika ukuaji wa uchumi wa soko na kumlinda mtumiaji, hivyo inahitajika nguvu ya pamoja Ili kuweza kuinua taifa katika misingi ya uchumi na uzalishaji, viwanda na uwekezaji"- amesema Mgasa