Dar es Salaam. Katika kuboresha huduma zake kwa wateja, Benki ya Exim Tanzania leo Jumatano imezindua huduma mpya zinazolenga kuhamasisha wateja wake na jamii kuhusu uwapo wa akaunti zake mpya tatu zinazofahamika kama akaunti ya ‘Haba na Haba’, ‘Haba na Haba Plus’ na akaunti ya ‘Mzalendo’.
Akaunti zote hizo zinalenga kuwawezesha wateja hao kuhifadhi fedha bila makato ya mwezi kwa matumizi ya kuweka akiba na kwa shughuli za kila siku.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hizo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Amana wa Benki ya Exim Tanzania, Agnes Kaganda alisema huduma hizo zinalenga wateja wote wakiwamo wenye kipato cha chini, kati na kipato kikubwa.
“Akaunti hizi zinalenga kukidhi mahitaji ya wateja ambao wanahitaji kuhifadhi fedha zao kwa matumizi ya siku zijazo. Huduma zote zimelenga kutatua changamoto ya ukosefu wa namna iliyo bora ya kuhifadhi fedha miongoni mwa Watanzania walio wengi bila kuwa na akiba isiyopungua makato ya kila mwezi,’’ alisema.
Pia Soma
- Mfanyabiashara akiri makosa, ahukumiwa kulipa Sh100 milioni
- Sh160 bilioni zanyenyuka Kenya
- Rais Museveni aamuru waliokamtwa kwa uvivu na uchafu waachiwe
Akizungumza kuhusiana na akaunti ya Haba na Haba Plus, Agnes alisema inawalenga watu wenye kipato cha juu ambao pia kupitia akaunti hiyo, wataweza kunufaika na viwango vikubwa vya riba. |