Tajiri namba Moja Duniani, Elon Musk anakabiliwa na uchunguzi kuhusu maelezo yake kununua hisa Twitter, huku wadhibiti wa shirikisho wakisema alichelewa kuwasilisha fomu muhimu katika mchakato huo, Jarida la Wall Street limeripoti.
Tajiri namba Moja Duniani, Elon Musk anakabiliwa na uchunguzi kuhusu maelezo yake kununua hisa Twitter, huku wadhibiti wa shirikisho wakisema alichelewa kuwasilisha fomu muhimu katika mchakato huo, Jarida la Wall Street limeripoti. Kanuni za Tume ya Usalama na Ubadilishanaji (SEC) zinahitaji wenyehisa kufichua hadharani wanapofikia asilimia 5 ya hisa za umiliki katika kampuni. Musk alifanya hivyo, lakini ilikuwa Aprili 4 ikiwa ni siku 10 baada kutakiwa kufanya hivyo.