Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dk Ndumbaro atoa neno kwa wawekezaji utalii

Ndumbaropicc Data Ndumbaro akitoa neno

Thu, 31 Mar 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Damas Ndumbaro amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa sekta ya utalii pamoja na kuendelea kuboresha huduma za kitalii nchini ikiwamo upatikanaji wa leseni ya shughuli za utalii kwa uharaka zaidi pamoja na mifumo ya malazi.

Pia, Dk Ndumbaro amesema Wizara ya Maliasili na Utalii itaendelea kutoa fursa katika maeneo yaliyohifadhiwa kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi.

Dk Ndumbaro amesema  hayo  leo Alhamisi jijini Dares Salaam wakati akikabidhi vyeti kwa wawekezaji waliokidhi vigezo na  kufanikiwa kupata maeneo ya uwekezaji mahiri katika maeneo ya wanyamapori (SWICA)yanayosimamiwa na  Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (Tawa) ambao ni  kampuni mbili  za  Grumet  Services Ltd pamoja na Mwiba Holding LTD.

Amewasisitiza wawekezaji wazawa pamoja na wa kigeni kulinda na kutangaza utalii na maeneo ya uhifadhi na vivutio hapa nchini, katika maeneo waliyopewa kuwekeza kwa kushirikiana na Serikali.

Pia Waziri Ndumbaro ametumia fursa hiyo kuwahamasisha wawekezaji wa kigeni kuwekeza nchini, akiitaja Tanzania kuwa ni salama, yenye amani na demokrasia na kwamba Wizara anayoiongoza imefungua milango kwa wawekezaji wote kuja kuwekeza nchini.

Advertisement “Sisi kama Wizara ya Maliasili na Utalii, falsafa yetu ni moja tu, mteja ni mfalme. Ndio maana mimi, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, tuko tayari kukutana na mwekezaji wa aina yoyote yule, muda wowote ule kujadili changamoto zozote zile, milango iko wazi,” amesema.

Dk Ndumbaro ameipongeza Tawa kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kulinda na kuhifadhi rasilimali za Taifa akisema kuwa Taasisi hiyo ni changa kuliko Taasisi zingine lakini wanafanya kazi ngumu na mazingira magumu zaidi ila wanafanya vizuri.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi Tawa, Meja Jenerali mstaafu Hamis Semfuko, ameishukuru Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Maliasili na Utalii, kwa kuipatia Tawa Sh12.9 bilioni ili kutekeleza miradi ya miundombinu ya utalii kupitia kampeni ya Maendeleo ya Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya Uviko-19.

Amesema miradi  hiyo inaendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye maeneo ya SWICA huku akithibitisha kuwa Tawa imeweka mipango madhuhuti, kuhakikisha miradi yote ambayo imekusudiwa kutekelezwa kwa kutumia fedha hizo inatekelezwa ndani ya muda uliopangwa na kwa ubora uliokusudiwa.

Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa vyeti hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Grumeti Reserves Ltd, Graham Ledger amesema kampuni ya Grumeti inashukuru kupata cheti cha umiliki wa vitalu viwili kwa sasa na  inaahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kulinda na kuendeleza shughuli za uhifadhi nchini

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Mark Ghaui ameishukuru Serikali kwa juhudi inazofanya kuhakikisha shughuli za uhifadhi zinaleta tija kwa Taifa  kwa kuhakikisha uhifadhi unaimarika kwa kuleta faid ya moja kwa moja kwa maisha ya wananchi kwa kupitia uwekezaji huo wa muda mrefu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live