Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dk Abbas asema sekta ya madini Tanzania imeonyesha mwanga

60543 Madini+pic

Thu, 30 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Serikali imesema Sh302. 63 bilioni zimekusanywa katika sekta ya madini kuanzia Julai Mosi, 2018 hadi sasa, kiasi  ambacho hakijawahi kukusanywa katika sekta hiyo.

Hayo yameelezwa leo Alhamisi Mei 30, 2019 na msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas katika mkutano wake na waandishi wa habari, akibainisha kuwa mafanikio hayo yametokana na mageuzi yaliyofanywa na Serikali iliyopo madarakani.

Amesema mabadiliko hayo yameipa heshima Tanzania na kuifanya kuwa mfano kwa nchi ya Afrika katika kuwabana wanyonyaji walioweka mizizi kwenye sekta hiyo.

“Watafiti wengi wanafanya tafiti kujua ni namna gani Tanzania imefikia hatua hiyo. Kuna nchi nyingi zimeanza kufuata nyayo zetu kwa kifupi tumejiwekea heshima kubwa,” amesema Dk Abbas.

Amesema siri kubwa ya mafanikio hayo ni kuongeza usimamizi, ufuatiliaji na kuwekwa mifumo ya kisayansi.

Licha ya kuanzishwa ndani ya muda mfupi masoko ya madini katika mikoa mbalimbali nchini yametajwa kuwa na mchango mkubwa katika sekta hiyo na kuzuia mianya ya utoroshaji wa madini vitendo vilivyokuwa vinaminya mapato ya Serikali.

Pia Soma

Kuhusu mfumo wa kufuatilia mawasiliano ya simu na miamala ya fedha (TTMS), Dk Abbas amesema umeonyesha mafanikio kwani tangu kuanza kwake umeingiza Sh97.16 bilioni fedha ambazo Serikali ilikuwa haizipati awali.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz