Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Senyi Ngaga ametoa saa 24 kwa machingi waliorudu barabarani kuondoka la sivyo watakutana na mkondo wa sheria
Ametoa agizo hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani humo.
Amesema Serikali imesha toa maelekezo kuwa machinga kutengewa maeneo na serikali ya wilaya imekwisha toa maeneo na machinga wote walihamia huko anashangazwa na baadhi ya machinga wanaorudi barabarani.
“Maeneo tulishatenga ninashangaa kinachowarudisha barabarani sikuoni naomba mrudi kwenye maeneo mliyotengewa" amesema Senyi.
Kulwa Shilingi mkazi wa Sengerema amesema wananchi wanatakiwa kifuata maelekezo ya Serikali ili kuondoka mkanganyiko unaoweza kujitokeza.