Menu ›
Biashara
Tue, 13 Apr 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
#HABARI: Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema utalii ni miongoni mwa sekta za kiuchumi zilizokumbwa na changamoto ya ukuaji kwa mwaka 2020/21 kutokana na janga la corona.
Majaliwa amesema hayo leo Bungeni Dodoma wakati wa mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
Ametaja baadhi ya hatua zilizochukuliwa na mataifa mengine duniani ili kujikinga ni pamoja na kufunga mipaka, kusitisha safari za ndege na kuwafungia watu ndani. Amesema hatua hizo zilichangia kutokua vizuri kwa sekta hiyo
Chanzo: www.habarileo.co.tz