Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Corona : Msimamo wa Waziri wanaouza Ndoo bei juu

Manyanyaaa Corona : Msimamo wa Waziri wanaouza Ndoo bei juu

Mon, 4 May 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Stella Manyanya ameelekeza Viwanda ya plastiki nchini kuzalisha ndoo kwa wingi na ametoa onyo kali kwa wafanyabishara wanaouza bei za juu vifaa vya kunawia mikono.

Amevipongeza Viwanda vyote kwa kwa kuendele kuzalisha ndoo na Vifaa vingine kwa wingi vinavyotumika kunawia mikono ambavyo vinahitajika sana katika kipindi hiki cha mapambano dhidi ya ugojwa wa Corona

“Nawapongeza na nimefurahishwa sana na uzalishaji mzuri na hakuna wasiwasi kwamba tutakuwa na upungufu wa ndoo za kunawia mikono katika maeneo yetu maana nimejionea uzalishaji mkubwa unaoendelea na ambao utaweza kukidhi maahitaji ya watanzania ya upatikanaji wa ndoo za kunawia mikono”

Aidha, ametoa onyo kali kwa wafanyabiashara wanaendelea kuuza bei Kubwa ndoo na vifaa vingine vya kunawia mokono kwa kufanya mapambano ya ugojwa huu kuwa fursa kwao ya kujinufaisha maradufu na kujipatia kipato kikubwa tofauti na ilivyokuwa awali.

“Natoa onyo kwa wafanyabiashara wote hasa wa reja reja kuna baadhi yao ambao wanatumia muda huu wa mapambano ya Corona kama fursa ya kujinufaisha maradufu, Ni marufuku kwa mtu yeyote kuongeza bei kupita kiasi maana kuna wafanyabishara wanaongeza mara mbili ya bei walizonunulia kiwandani”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live