Jamii imehimizwa kuchangamkia frusa za kibiashara zinazopatikana katika nishati safi ya kupikia hatua ili kupunguza athari za uharibifu wa mazingira zinazotokana na matumizi ya mkaa na kuni.
Akizungumza katika kongamano la nishati safi ya kupikia lililoandaliwa na taasisi ya wanawake wafanyabishara Tanzania (TABWA), Meneja masoko wa kampuni ya gesi ya Oryx, Peter Ndomba, amesema fursa ni kubwa katika biashara hiyo.
Amesema kwa sasa watumiaji wa nishati safi ya kupikia ni asilimia tano na kwamba lengo la serikali ni kufikisha watumiaji zaidi ya asilimia 80 kwa miaka kumi ijayo na hivyo fursa bado ni kubwa kwa wajasiriama kuwekeza katika biashara hiyo.