Serikali inakamilisha ujenzi wa boti za uvuvi 150 zitakazopelekwa kwa wavuvi katika maeneo mbalimbali nchini, ili kusaidia wavuvi katika shughiuli zao na kupata matokeo chanya kwenye shughuli zao.
Serikali inakamilisha ujenzi wa boti za uvuvi 150 zitakazopelekwa kwa wavuvi katika maeneo mbalimbali nchini, ili kusaidia wavuvi katika shughiuli zao na kupata matokeo chanya kwenye shughuli zao. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi David Silinde ameliambia Bunge jijini Dodoma kuwa ujenzi wa boti hizo upo katika hatua za mwisho na kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha zitakuwa zimekamilika na kupelekwa kwa wavuvi.