Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bodi ya Wakurugenzi TRA yafurahishwa uwekezaji wa SBL

TRA Uledi Sehemu ya bodi ya TRA ikisikiliza maelezo toka kwa Mtendaji Mkuu wa SBL

Tue, 15 Mar 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetembelea kiwanda cha bia cha Kampuni ya Serengeti (SBL) cha Dar es Salaam na kuelezea kuridhishwa na uwekezaji inayofanya kampuni hiyo hapa nchini.

Akiongea katika ziara hiyo iliyolenga kuangalia namna zoezi la utekelezaji wa stempu za kielekroniki unavyoendelea, mwenyekiti wa bodi hiyo Ulledi Mussa alisema uwekezaji unafanywa na SBL unatija kubwa kwa taifa.

“Upanuzi mkubwa wa viwanda vyenu unaonyesha kuwa mpo na mtanendelea kuwepo. Serikali ipo Nyuma yenu na changamoto mbali mbali za kikodi zzitakuwa zikendelea kufanyiwa kazi ili kuwawekea mazingira mazuri zaidi ya kufanya kazi,” alisema

Mwenyekiti huyo alisema kuwa TRA inaichukulia kampuni ya SBL km mdau muhimu wa maendeleo na kushukuru kwa uwekezaji wake katika miradi mbali mbali ya kijamii.

Kwa upande wake, mkurugenzi wa mahusiano kwa umma wa SBL John Wanyancha alisema kampuni hiyo imekuwa ikiwekeza katika midari mbali mbali ya kijamii kama vile maji, elimu, Kilimo endelevu na nyinginezo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live