Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

BoT yamuondoa Nyabundege TIB Corporate

66733 TIB+PIC

Sun, 14 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Kutokana na mwenendo usioridhisha wa Benki ya TIB Corporate, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesitisha uteuzi wa, Frank Nyabundege aliyekuwa mkurugenzi mtendaji kuanzia Julai 13, 2019.

BoT imetumia mamlaka iliyonayo kwa mujibu wa sheria ya benki na taasisi za fedha ya mwaka 2006 kusimamisha ukurugenzi wa Nyaundege aliyeiongoza benki hiyo tangu Agosti Mosi, 2014.

“Hatua hizi zina lengo la kuboresha usimamizi na utendaji wa benki zinazomilikiwa na Serikali. Benki Kuu ya Tanzania inauhakikishia umma kuwa Benki ya TIB Corporate itaendelea kutoa huduma na madai yote yaliyoiva yatalipwa kama kawaida,” inasomeka sehemu ya taarifa iliyotolewa na BoT.

BoT imeeleza kuwa imechukua uamuzi huo kutokana na mwenendo usioridhisha wa TIB Corporate na imemteua Fred Luvanda kutoka kurugenzi yake ya usimamizi wa sekta ya fedha kuwa kaimu mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo.

BoT imesema itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika benki kuhakikisha sekta ya fedha inakuwa stahimilivu na kuchangia maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Kuondolewa kwa Nyabundege kumefanywa baada ya BoT kuzifunga benki kadhaa ndani ya miaka minne iliyopita katika maeneo tofauti nchini huku baadhi zikilazimishwa kutafuta wabia wa kuungana nao kutokana na mwenendo usiridhisha.

Pia Soma

Benki ya Twiga ililazimika kuungana na Benki ya Posta (TPB) huku Benki M, Benki ya Wananchi Mbinga, Meru na Njombe pamoja na Benki ya Ushirika Kagera na Efatha zikifungwa kutokana na kutokidhi viwango vya BoT.

BoT inadhamana la kumthibitisha mtu yeyote anayependekezwa na bodi ya wakurugenzi kuwa mkurugenzi mtendaji wa benki au taasisi yoyote ya fedha nchini.

Chanzo: mwananchi.co.tz