Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Sauda Kassim Msemo amesema katika kutatua changamoto za huduma jumuishi za fedha nchini, sekta ya fedha itasimamia katika kuanzisha mikakati mbalimbali kwa kuweka mifumo thabiti ya usimamizi.
Ameongeza kuwa mifumo thabiti ya TEHAMA nayo itawekwa kwa ajili ya kutatua changamoto ambazo Wananchi wanazipata, na kuandaa kanuni mbalimbali ambazo zitaweza kuweka unafuu wa kupata huduma za fedha ili kuongeza wigo wa Wananchi kupata huduma hizo.
Naibu Gavana huyo wa BOT alikuwa akizungumza mkoani Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa mkakati wa Taifa wa Huduma Jumuishi za Fedha.