Serikali imeridhia pendekezo la kuvunja Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TaDB) na kuiunganisha na Mfuko wa Pembejeo za Kilimo (AGITF) ikiwa ni sehemu ya maamuzi yaliyoshuhudia mashirika mengine 14 yakivunjwa na kuunganishwa ili koongeza ufanisi.
Serikali imeridhia pendekezo la kuvunja Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TaDB) na kuiunganisha na Mfuko wa Pembejeo za Kilimo (AGITF) ikiwa ni sehemu ya maamuzi yaliyoshuhudia mashirika mengine 14 yakivunjwa na kuunganishwa ili koongeza ufanisi. Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof Kitila Mkumbo ametangaza leo Ijumaa Disemba 15, jijini Dar es Salaam kuwa lengo la mpango huo ni kuwezesha kuwa na taasisi moja itakayohusika na mikopo na ugharamiaji wa maendeleo ya kilimo nchini.